Juzi ikiwa ni siku ya wapendanao, Mbunifu wa mavazi mahiri nchini Asia Idarious aliandaa onesho lake la mavazi ambapo pia liliendana na maadhimisho ya miaka 10 ya onesho hilo lijulikanalo kama Lady in Red.
Tukio hilo lilifanyika katika Hotel ya Serena na iliendana na burudani safi kutoka kwa kundi la sanaa la Wanne Star pamoja na msanii Nyemo.
Michuzi Blog ilikuwa ni moja kati ya wadhamini wakubwa huku kukiwa na wadhamini wengine kama vile kampuni ya TDL kupitia kinywaji chake cha Zanzi.
Ilikuwa ni onesho zuri lililowakutanisha pamoja wabunifu wakongwe wa mitindo pamoja na wabunifu chipukizi na pia iliendana sambamba na mnada kuchangisha fedha za kuwasaidia waathirika wa madawa ya kulevya. Kwa habari zaidi ingia blog ya www.habari5.blogspot.com